Rubiales atiwa hatiani Uhispania kwa kulazimisha busu
20 Februari 2025Waendesha mashtaka walikuwa wameomba kifungo cha miaka miwili na nusu jela kwa Rubiales -- mwaka mmoja kwa unyanyasaji wa kingono na miezi 18 kwa shtaka la kulazimisha -- kwa madai ya kumshinikiza mchezaji huyo kutozungumzia kitendo hicho.
Rubiales alishtakiwa kwa unyanyasaji wa kijinsiakwa kumbusu Hermoso mnamo 2023 kufuatia ushindi wa Uhispania katika Kombe la Dunia la Wanawake nchini Australia, na vile vile kulazimisha kwa madai ya kujaribu kumshawishi kupuuza tukio hilo baadaye.
Shutuma zilizozuka kufuatia tukio hilo la busu zilimlazimu Rubiales kujiuzulu kwa fedheha na kutilia mkazo juu ya kuenea kwa utamaduni wa mfumo dume na ubaguzi wa kijinsia katika michezo.
Hermoso, 34, alisema siku ya ufunguzi wa kesi hiyo mnamo Februari 3 kuwa alihisi "kudharauliwa" baada ya busu lisilo la ridhaa ambalo "halipaswi kutokea katika mazingira yoyote ya kijamii au ya kazi".
Lakini Rubiales, 47, aliiambia mahakama siku ya Jumanne kuwa "ana uhakika kabisa" Hermoso alikubali busu hilo alipokuwa akipanda jukwaani kupokea medali yake ya ushindi, tukio lililorushwa moja kwa moja duniani kote, na akakana kumshinikiza kutozungumzia kisa hicho.
Alikubali "alifanya makosa" kwenye jukwaa, akisema alipaswa "kuwa na jukumu la kitaasisi zaidi", lakini akakana kuwa kosa lolote lilifanyika.
afp