Wanariadha wa Afrika Mashariki wakabiliwa na unyanyasaji
19 Juni 2025Matangazo
Watafiti wa ripoti hiyo wailiwahoji watu zaidi ya 700, wengi wao wakiwa na umri kati ya miaka 18-34 na ambao ni wanariadha kitaaluma na walioshiriki mashindano ya kitaifa au kimataifa. Katika miaka ya hivi karibuni kumeripotiwa vifo na mauaji ya wanariadha mashuhuri wa kike nchini Kenya.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa unyanyasaji wa kijinsia na kingono umekita mizizi katika sekta ya michezo huko Afrika Mashariki kutokana na mpangilio duni unaochochewa na mitazamo ya mfumo dume, kutoadhibiwa kwa wahalifu na utamaduni wa kukaa kimya kwa wahanga.