Ripoti:Mashambulizi ya Marekani hayakuharibu nyuklia ya Iran
25 Juni 2025Matangazo
Hayo yamebainishwa katika ripoti mpya ya tathmini iliyofanywa na idara ya Ujasusi katika wizara ya Ulinzi wa Marekani.
Vyanzo vitatu vinavyofahamu suala hilo na ambavyo vilizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, vimeliambia shirika la habari la Reuters kwamba hifadhi ya madini ya urani yaliyorutubishwa ya Iran haikutokomezwa na kwamba mpango wa nyuklia wa nchi hiyo umecheleweshwa kwa mwezi mmoja au miwili pekee.
Hayo yanajiri wakati kukishuhudiwa utekelezwaji legelege wa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Iran ambazo zote zimejinadi kuwa washindi katika mzozo huo. Hata hivyo waangalizi wengi wanasubiri kushuhudia hatma ya mzozo huo wa Mashariki ya Kati.