Rice: Arsenal ina uwezo wa kuitupa nje PSG
7 Mei 2025Matangazo
Gunner hii leo watakuwa ugenini mjini Paris kwa nusu fainali ya pili wakiwa na matumaini ya kujikomboa baada ya kushindwa nyumbani Emirates 1-0 bao likitiwa kimyani na Ousmane Dembele.
Soma pia: Inter yasaka ukombozi wa ligi ya mabingwa Ulaya
Licha ya kuonyesha mchezo mzuri katika nusu fainali ya kwanza, Rice anasisitiza kwamba Arsenal "wasiwe na hofu" wanaweza kuwakabili PSG na kufuzu kwa fainali yao ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa katika takriban miongo miwili.
Mshindi katika mechi ya leo atakutana na Inter Milan ambao hapo jana waliicharaza Barcelona 4-3 na kujihakikishia nafasi ya fainali.
Dembele aondoa hofu ya jeraha baada ya kutolewa uwanjani dhidi ya Arsenal