Ureno: Mahakama iingilie kati sheria kali ya uhamiaji
25 Julai 2025Sheria hiyo inawawekea vikwazo wahamiaji wanaotaka kuleta familia zao na kupunguza njia za kukata rufaa iwapo maombi yao ya kuishi yatafutiliwa mbali, hatua ambayo rais amesema inakiuka misingi ya usawa na kutokubaguliwa.
Mawaziria mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wajadili uhamiaji
Kupitia taarifa aliyotoa Alhamisi usiku mjini Lisbon, rais de Sousa aliitaka mahakama kutoa uamuzi wa haraka ndani ya wiki mbili, huku akielezea kuwa sheria hiyo pia inakinzana na haki ya kuunganishwa kwa familia na maslahi ya mtoto.
Wakati chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha Chega kikipinga hatua hiyo ya rais, vyama vya mrengo wa kushoto viliunga mkono uamuzi huo. Ureno kwa sasa ina wahamiaji milioni 1.55 wengi wao wakitokea Brazil, Uingereza, Italia na Ufaransa.