Rais wa Sudan Kusini amfuta kazi Waziri wa Fedha
22 Agosti 2025Redio ya taifa pia imeripoti kwamba Kiir amemwondoa waziri wa uwekezaji.
Hatua hizi zinakuja wakati taifa hilo likikabiliwa na changamoto kubwa za kiuchumi, ikiwemo kuporomoka kwa mapato ya mauzo ya mafuta ghafi tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe vya 2013–2018, na hivi karibuni, usumbufu katika usafirishaji kutokana na vita nchini Sudan.
Umoja wa Mataifa watahadharisha juu ya maafa huko Sudan
Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) linakadiria uchumi wa Sudan Kusini utakua kwa kiwango hasi cha asilimia 4.3 mwaka 2025, huku mfumuko wa bei ukipanda hadi asilimia 65.7
Hali hii inazua hofu ya kuongezeka kwa mivutano ya kisiasa, hasa baada ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Riek Machar, kuwekwa kizuizini Machi mwaka huu, hatua ambayo serikali inasema ililenga kuzuia uchochezi wa vurugu na kuhujumu amani kuelekea uchaguzi ujao.