SiasaMarekani
Trump asaini amri itakayozuia waliojibadili jinsia jeshini
28 Januari 2025Matangazo
Rais Trump ambaye alijaribu kuchukua uamuzi kama huo wakati wa muhula wake wa kwanza lakini akakabiliwa na vikwazo vya kisheria, amesema hatua hiyo itahakikisha Marekani inakuwa na jeshi imara zaidi duniani.
Katika mfululizo wa maagizo mengine kuhusiana na jeshi, Trump ametoa pia wito wa Marekani kuanzisha mfumo wake wa ulinzi wa makombora unaoshabihiana na mfumo wa ulinzi wa anga wa Israel.
Hatua hii inapingwa na wanaharakati wa jamii za watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja ambao wanaiona kama ukiukwaji wa haki za binaadamu.