Rais wa Korea Kusini Lee Myung yuko Japan kwa ziara rasmi
23 Agosti 2025Matangazo
Lee pia anatarajiwa kukutana na rais wa Marekani Donald Trump mjini Washington siku ya Jumatatu wiki Ijayo.
Katika ziara yake ya kwanza rasmi Japan, Lee atakutana na Waziri Mkuu Shigeru Ishiba ofisini mwake mjini Tokyo, kujadili kuhusu uhusiano wao wa pamoja ikiwemo ushirikiano wa karibu wa usalama na Marekani chini ya mkataba ya pande tatu uliotiwa saini na watangulizi wao.
Korea Kusini lazima ijiondoa katika mitego ya Marekani
Mikutano hiyo inafanyika baada ya Korea Kusini na Japan kufikia makubaliano ya kibiashara yaliyowaepusha na ushuru mkubwa uliopangwa na Marekani, kwa masharti ya kuwekeza mabilioni ya dola katika miradi mipya nchini humo.