MigogoroMashariki ya Kati
Vita vya Iran na Israel: Rais wa Iran alinusurika kuuawa
13 Julai 2025Matangazo
Ripoti ya shirika hilo imeeleza kuwa jeshi la Israel lililipua jengo la Usalama wa Taifa, siku tatu baada ya vita kuanza.
Miongoni mwa waliokuwemo kwenye jengo hilo katika mkutano wa kukabiliana na mgogoro huo alikuwa Rais Pezeshkian. Licha ya washiriki wote kutoka salama nje ya jengo hilo, baadhi yao akiwemo kiongozi huyo walipata majeraha miguuni.
Wakati huohuo, Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Iran Abbas Araghchi amebainisha kuwa Tehran itakuwa tayari kurejea kwenye mazungumzo ya nyuklia na Marekani ikiwa tu itahakikishiwa kwamba haitashambuliwa tena.