Chad yakaribisha hatua ya Ufaransa kujiondoa nchini humo
31 Januari 2025Matangazo
Deby amesema hayo alipowatubia wanajeshi wa Chad na wanadiplomasia siku moja baada ya kukamilika kwa makabidhiano ya kambi ya mwisho ya Wafaransa ya Kossei.
Makabidhiano hayo yanafuatia hatua ya ghafla ya Chad ya kuvunja uhusiano wa kijeshi na mkoloni wake huyo wa zamani, Novemba mwaka uliopita.
Soma pia:Chad yasema shambulio lililotibuliwa lilifanywa na walevi
Lakini Deby amesema hiyo haiondoi uhusiano wao na Ufaransa, bali inahusiana tu eneo la kijeshi.
Ameongeza kuwa, Chad sasa inalazimika kujenga jeshi lenye nguvu zaidi na lenye vifaa bora zaidi na "kuanzisha ushirikiano mpya wenye msingi wa kuheshimiana na bila kupoteza mwelekeo wa matakwa ya uhuru na mamlaka.