MigogoroUrusi
Rais Vladimir Putin atangaza usitishwaji wa mapigano
28 Aprili 2025Matangazo
Usitishwaji huo wa mapigano utakwenda sambamba na kumbukumbu ya miaka 80 ya ushindi dhidi ya Wanazi wa Ujerumani.
Taarifa ya Ikulu ya Kremlin imesema katika kipindi hicho, mapigano yote yatasimamishwa na aliyechukua maamuzi hayo kwa misingi ya kiutu.
Amesema, Urusi inadhani ni muhimu Ukraine nayo ikafuata mfano huo. Ukraine lakini bado haijasema chochote kuhusu hatua hii.
Hatua hiyo inachukuliwa wakati Rais wa Marekani Donald Trump anayetaka kumalizwa kwa vita vya miaka mitatu nchini Ukraine, akionyesha kuchukizwa na mashambulizi yanayofanywa na Putin katika siku za karibuni na kumtaka kuacha mara moja.